/* That's all, stop editing! Happy blogging. */

Joto Lazidi Kupanda....UKAWA Wafungua Kesi Mahakamani Kupinga Wananchi Kuzuiwa Kulinda Kura Soma Zaidi hapa


Leo tarehe  16 October 2015, Ukawa kupitia wakili wa CHADEMA,Peter Kibatala na mawakili wengine, wamefungua chini ya hati ya haraka sana (certificate of extreme urgency) shauri nambari 37 la mwaka 2015 katika Mahakama Kuu ya Tanzania (Main Registry) wakiomba Mahakama Kuu itoe tafsiri sahihi ya kifungu cha 104 (1) cha Sheria ya Uchaguzi Tanzania na itamke iwapo wapiga kura na watu wengine wenye shauku wanaruhusiwa au la kukaa KWA UTULIVU umbali unaozidi meter 200 kutoka kituo cha kupigia kura/kufanya majumuisho ya kura.
Pia wameiomba Mahakama Kuu itamke iwapo ni halali kwa Rais wa nchi kutoa matamko aliyoyatoa kwa namna ya katazo kwa wapiga kura/raia wenye shauku kukaa KWA UTULIVU umbali unaozidi mita 200 kutoka kituo cha kupigia kura/kufanya majumuisho.
Pia wameiomba Mahakama Kuu itamke iwapo Rais ana mamlaka hayo kisheria kwa kuzingatia Sheria ya Uchaguzi Tanzania.

Taarifa  hii  ni  kwa  mujibu  wa  Wakili  Peter  Kibatala  ambaye  ameshare  nasi  kwenye  ukurasa  wake  wa  facebook 

Newer Posts Older Posts
© Copyright BONGO CLASIC Published.. Blogger Templates
Back To Top