
Mgombea urais kupitia chama cha TLP 
Macmillan Lyimo amesema anaunga mkono kauli ya mwenyekiti wake wa chama 
Mh. Augustine Mrema ya ‘kumpigia debe’ mgombea wa chama cha mapinduzi 
CCM, Dk John Magufuli, kwa madai kuwa hayo ni maamuzi yake binafsi.
Akizungumza na EATV, Lyimo amesema kuwa 
kauli hiyo haijatolewa na mkutano wowote wa chama, bali ni maoni binafsi
 kwa kuwa mwaka huu watanzania wanachagua mtu na siyo chama na kwamba 
jambo alilofanya Mrema si jipya wa la ajabu.
“Hili jambo siyo la ajabu, hata 
Marekani, Colin Powell alitangaza kumuunga mkono Obama licha ya kuwa 
chama tofauti, Mrema amesema hivyo kwa kuwa anajua looser siyo yeye, 
tumesimamisha wagombea ubunge nchi nzima, na yeye ni mmoja wapo, kwahiyo
 hilo halinipi shida” Amesema Macmillan Lyimo
Kuhusu mahusiano kati yake na mwenyekiti
 huyo, Lyimo amesema kuwa mahusiano ndani ya chama hicho ni mazuri na 
hakuna ugomvi wowote.
“Tunaendelea kushirikiana kama kawaida, na hata kampeni zangu nilianzia kwake na nitafungia jimboni kwake” kauli ya Lyimo
Kuhusu nafasi yake ya ushindi, Lyimo amesisitiza kuwa yeye ndiye atakayeshinda urais mwaka huu, na kamwe Rais hatoki CCM
“Magufuli hawezi kushinda, nafasi kubwa 
ya ushindi ninayo mimi, hata Magufuli anajua kuwa mimi napinga huo 
mwenge kwenye picha yake, hiyo ni ishara ya uchawi, na uchawi wake 
utashindwa mwaka huu”. Amesema mgombea huyo
 


 
 
 
 
 
 
